SPORTS


Taarifa mpya kuhusu ushindi wa Miss Tanzania 2014, Sitti Mtemvu


Screen Shot 2014-11-08 at 7.49.07 PM
Lilian ambae ndio amevishwa taji hilo kwa sasa ni kwa kwanza kutoka kulia.
Tangu Sitti Mtemvu atangazwe mshindi pale Mlimani City kumekua na malalamiko kutoka kwa baadhi ya Watanzania yalifuatia kutokana na umri wake pamoja na taarifa nyingine ambazo yeye alizikanusha na kusema ni uzushi ikiwemo ya kuwa na mtoto.
Baada ya haya yote Novemba 8, 2014 Kamati ya Miss Tanzania imekutana na waandishi wa habari Dar es salaam na kutangaza kwamba Sitti Mtemvu ameandika barua kwa hiari yake yeye mwenyewe, kwamba amelivua taji hilo hivyo kamati hiyo ikamtangaza ambaye atashikilia taji hilo kwamba ni mshindi namba mbili wa Miss Tanzania 2014 Lilian Kamazima.




Museveni agharamia Uganda Cranes

Rais Yoweri Museveni wa Uganda amegharamia safari ya timu ya soka ya taifa Uganda Cranes kwenda Togo, kucheza mechi ya marudiano siku ya jumatano ya kufuzu kucheza fainali ya kombe la mataifa ya Afrika mwaka 2015 kundi E.
Msemaji wa Shirikisho la soka nchini Uganda Ahamed Hussen amefahamisha BBC kwamba Rais Museveni amewapatia dolla laki moja na efu arobuni kusafirisha timu ya Uganda Cranes kwenda Togo kwa mechi ya Jumatano.
Hicho ni kikosi cha Uganda Cranes kilichovalia jezi nyekundu yaani yenye kuishia 42 na yenye 40 ni Togo.
Katika mechi ya jumasi Uganda Cranes ilinyamazishwa na Togo kwa bao 1 kwqa nunge hivyo Uganda wanahitaji ushindi mechi ya Jumatano kuongeza matumaini ya nafasi ya kushiriki fainali ya kombe la Afrika mwaka 2015 nchini Morocco.
Katika kundi hilo E Ghana ndiyo wanaongoza na alama 5 wakifatiwa na Uganda alama 4, Ginea alama 4 na Togo alama 3


No comments:

Post a Comment